Tuesday, April 2, 2019

Waziri Biteko awasimamisha kazi Maafisa Madini Ofisi ya Madini Chunya


Na Tito Mselem, Chunya

Waziri wa Madini Doto Biteko amewasimamisha kazi Maafisa Madini wote wa Ofisi ya Madini Chunya Mkoani Mbeya na kuteua Wajiolojia watakaokaimu nafasi hizo wakati wizara ikitafuta Maafisa wengine waaminifu watakaofanya kazi hizo.

Hatua hiyo imekuja baada ya kugundua wizi mkubwa wa madini ya dhahabu unaofanywa na maafisa hao wakishilikiana na wamiliki wa kampuni ya uchenjuaji wa dhahabu.

Akizungumza katika mkutano na wachimbaji wadogo wadogo pamoja na wamiliki wa makampuni ya uchenjuaji wa dhahabu Waziri Biteko, amesema udanganyifu unaofanywa na Maafisa hao wa Madini pamoja wenye  kampuni hizo za uchenjuaji ni mkubwa na  hahuitaji msamaha hata kidogo.

“Mimi kama Waziri mwenye dhamana katika sekta hii ya Madini ninawapenda sana wachimbaji ila nasikitika sana kwa wachimbaji na wenye makampuni ya uchenjuaji kutokuwa waaminifu,” amesisitiza Waziri Biteko

Ameongeza kuwa, Maafisa wa madini hao ndiyo wanaotoa mianya ya wizi wa dhahabu unaofanyika kwenye kampuni zaa uchenjuaji wa dhahabu  wilayani humo.

Aidha, katika ziara hiyo Biteko ameifunga kampuni ya   Ntorah Gold Company Ltd inayohusika na uchenjuaji wa dhahabu wilayani  humo baada ya kutoa taarifa za udanganyifu kwa serikali.

Pia, Waziri Biteko ameongeza kwamba, Wilaya ya  Chunya ndiyo sehemu pekee Tanzania inayoongoza kwa wizi wa dhahabu na kutoa taarifa za uongo za kampuni za uchenjuaji wa dhahabu ikifuatiwa na wilaya ya Kahama iliyopo Mkoani Shinyanga.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjla, amesema serikali imeondoa kodi zote kwa wachimbaji wadogo zilizokuwa zikilalamikiwa na wachimbaji pamoja na kampuni za uchenjuaji wa dhahabu lakini bado wizi unafanyika tena kwa kiwango kikubwa.  

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amikiri kwamba hana elimu ya madini hivyo imekuwa vigumu kwake kudhibiti wizi huo   lakini anaamini wizi na udanganyifu upo tena kwa kiwango kikubwa.

“kiukweli sina elimu ya madini hasa kwenye upande wa uchenjuaji wa dhahabu, naamini kuna wizi mkubwa wa madini haya ya dhahabu na taarifa zisizo na ukweli”amesema  Chalamila.


Baadhi ya Viongozi waandamizi wa Wizara ya Madini na Viongozi wengine wa Wilaya ya Chunya wakisikiliza maelezo ya namna wizi unavyofanyika katika mitambo ya kuchenjua dhahabu. 
Wachimbaji wadogo wadogo wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauli ya wilaya ya Chunya wakimsiliza Waziri wa Madini Doto Biteko


Waziri wa Madini Doto Biteko akitoa akieleza jambo wakati akitoa maelekezo ya namna ya kuifungia kampuni ya uchenjuaji dhahabu ya Ntorah Gold and Diamond Ltd wilayani Chunya

No comments:

Post a Comment