Monday, February 18, 2019

Wadau wa Tanzanite Mirerani waandamana kumpongeza Rais Magufuli


Ø NI KUFUATIA KUPUNGUZA KODI ZA MADINI NA KUSIKILIZA KERO ZAO

Ø WAAHIDI KULIPA KODI

Maandamamo hayo yaliyofanyika Februari 16, yalihusisha wadau wote wa madini ya Tanzanite wanaofanya shughuli za uchimbaji ndani ya ukuta wakiwemo wachimbaji wadogo, wa Kati na Wakubwa, yakilenga kumpongeza Rais Dkt. John Magufuli kwa kupunguza kodi za madini, kusisitiza suala la uanzishwaji wa masoko ya madini na  mwongozo wa uongezaji thamani madini

v ALIYOYASEMA MKUU WA MKOA WA MANYARA, ALEXANDER MNYETI
 Mhe. Rais ametuagiza mlipe kodi kwa hiari. Msipofanya hivyo mtalipa kwa nguvu. Lipeni kodi.

Ø Nimepokea maandamano yenu na tutaandaa barua Maalum kwenda kwa Mhe. Rais kufikisha salam zenu. 

Ø Mnajua safari ya tulikotoka, tulipofika na tunaweza kutengeneza njia nzuri ya tunakotaka kufika. MAREMA inakwenda vizuri.

Ø Mirerani acheni umbeya, kuna uongo mwingi, punguzeni uongo taarifa zenu zinatupotosha. 

Ø Mnajichonganisha wenyewe na serikali. Waajiri mnawatelekeza wafanyakazi wenu wakiugua wanakuwa mzigo wa serikali.

ALIYOYASEMA MWENYEKITI WA MAREMA, MKOA WA MANYARA, JUSTIN NYARI

Ø Maandamano haya yanalenga kutoa pongezi kwa Rais Magufuli kwa kuondo kodi ambazo hazikuwa rafiki kwa wachimbaji.Tunampongeza Mhe. Rais kwa  kupeleka bungeni Muswada kwa hati ya dharura, ujenzi wa masoko  ya madini na mwongozo wa uongezaji thamani madini.

Ø Wachimbaji wako tayari  kushirikiana na serikali kukuza uchumi kupitia sekta ya madini.

ALIYOYASEMA MBUNGE WA SIMANJIRO, JAMES OLLE MILLYA

Tunampongeza Rais kwa kuondoa VAT ya asilimia 18 kwenye sekta. Ameacha asilimia 7 tu huu ni upendo wa pekee.

Baada ya Januari 22 Mkuu wa Mkoa aliitisha kikao Januari 25 na migodi yote imeanza kufanya kazi na matunda yameanza kuonekana.

ALIYOYASEMA MKUU WA WILAYA YA SIMANJIRO, MHANDISI ZEPHANIA CHAULA

Ø Kama Mhe. Rais amewaheshimu na ninyi mumheshimu, heshima hiyo ni kulipa kodi.

ALIYOYASEMA MWAKILISHI WA TANZANITE AFRIKA KWA NIABA YA WACHIMBAJI WA KATI, WILFRED MUSHI

Ø Tunampongeza Mhe.Rais, kwa mara ya kwanza ameondoa kero za wachimbaji wa  Kati ambazo hazipishani sana na wachimbaji wadogo.

Ø Nuru ya Tanzanite imenga'rishwa,
Mirerani sasa inakwenda kutengeneza  tanzanite mpya.

ALIYOYASEMA MWAKILISHI WA TANZANITE ONE, FEISAL SHABHAI

Ø Tunampongeza Rais Magufuli kwa kutambua uwepo wetu, kusikiliza kilio chetu na kuondoa changamoto zetu.
Ø Tunatambua maendeleo yanayotarajiwa kutokana na rasilimali hii ambayo lengo ni kuwanufaisha watanzania na vizazi vijavyo viweze kuishi katika mazingira salama.

ALIYOYASEMA MWAKILISHI WA TAMIDA, HUSSEIN GONGA 

Ø Tulikuwa na tashwishi kubwa juu ya kufanya biashara ya madini. Mhe Rais alisikia kilio cha wachimbaji na dealers.

Ø Hawezi kuwepo mnunuzi bila mchimbaji, tulikuwa na changamoto ya kusafirisha madini ghafi.

Ø Rais Magufuli ameondoa kodi ya VAT ya asilimia 18, ilikuwa kero kubwa.

Ø Mhe. Rais hajapoteza, mafanikio  atayaona tunamhakikishia. Biashara ya madini  sasa inakuwa nzuri.

ALIYOYASEMA MWAKILISHI WA BROKER,
Ø Tunampongeza Rais kwa suala la ujenzi wa masoko ya madini nchi nzima, serikali itakusanya kodi ya kutosha.

Ø Niwaombe Ma broker, kufanya uthamini wa madini, sitamwombea radhi broker yoyote atakayevunja sheria.

ALIYOYASEMA MWAKILISHI WA WANA APOLLO

Ø Tunampongeza Rais Magufuli kwa kututambua wana Appolo na kutupa nafasi ya kuwasilisha kero zetu. Tunaahidi kushirikiana katika nyaja zote. Wana Appolo ndiyo wachimbaji wa tanzanite.

Ø Tunayo sababu ya kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Manyara, leo wana Appolo tunapewa vipaza sauti. Kwa muda mrefu wana Appolo hawakuwa na sehemu ya kuzungumza.






No comments:

Post a Comment