Friday, December 14, 2018

Waziri Kairuki, Waziri wa Maliasili China wafanya mazungumzo


Beijing, China

Waziri wa Madini Angellah Kairuki na Waziri wa Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa China LU Hao Desemba 11 walifanya mazungumzo Beijing, nchini China wakati Tanzania ikishiriki katika Jukwaa la Uwekezaji katika Sekta ya Madini nchini humo.

Waziri wa Maliasili ndiye anayesimamia masuala ya Madini nchini China.

Kufuatia mazungumzo hayo, Waziri wa Maliasili wa China aliona kuwa maombi  yaliyowasilishwa na Waziri Kairuki ni ya msingi hivyo, nchi hizo zimekubaliana kuwa na  Kundi la Pamoja  la  Kazi  kati  ya wizara hizo  mbili ambalo  litapitia na kuchambua maeneo ya ushirikiano na baadaye  nchi husika zitasainiana Mkataba wa Makubaliano.

Aidha, nchi hizo zimekubaliana kukuza ushirikiano katika maeneo ya utafiti, mafunzo na uwekezaji katika sekta ya madini.

Wizara ya Madini ilishiriki Jukwaa la Uwekezaji katika Sekta ya Madini tarehe 10 Desemba, mwaka huu Beijing nchini China. Jukwaa hilo liliandaliwa na Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kuwashirikisha wadau mbalimbali wa sekta ya madini nchini.


Waziri wa Madini Angellah Kairuki na Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa China, LU Hao wakipeana mikono baada ya kukamilisha mazungumzo.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akimkabidhi Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa China LU Hao, zawadi ya picha inayoonesha wanyama mbalimbali wanaopatikana nchini

Waziri wa Madini Angellah Kairuki na Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa China, LU Hao wakiwa katika kikao cha majadiliano baina yao.

No comments:

Post a Comment