Beijing, China
Waziri wa Madini Angellah Kairuki na
Waziri wa Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa China LU Hao Desemba 11 walifanya
mazungumzo Beijing, nchini China wakati Tanzania ikishiriki katika Jukwaa la
Uwekezaji katika Sekta ya Madini nchini humo.
Waziri wa Maliasili ndiye
anayesimamia masuala ya Madini nchini China.
Kufuatia mazungumzo hayo, Waziri wa
Maliasili wa China aliona kuwa maombi yaliyowasilishwa na Waziri Kairuki ni ya
msingi hivyo, nchi hizo zimekubaliana kuwa na Kundi la Pamoja la
Kazi kati ya wizara hizo mbili ambalo litapitia
na kuchambua maeneo ya ushirikiano na baadaye nchi husika zitasainiana
Mkataba wa Makubaliano.
Aidha, nchi hizo zimekubaliana kukuza
ushirikiano katika maeneo ya utafiti, mafunzo na uwekezaji katika sekta ya
madini.
Wizara ya Madini ilishiriki Jukwaa la
Uwekezaji katika Sekta ya Madini tarehe 10 Desemba, mwaka huu Beijing nchini
China. Jukwaa hilo liliandaliwa na Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Kituo
cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kuwashirikisha wadau mbalimbali wa sekta ya
madini nchini.
Waziri wa
Madini Angellah Kairuki na Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa China, LU Hao wakipeana
mikono baada ya kukamilisha mazungumzo.
|
Waziri wa
Madini Angellah Kairuki akimkabidhi Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa
China LU Hao, zawadi ya picha inayoonesha wanyama mbalimbali wanaopatikana
nchini
|
Waziri wa
Madini Angellah Kairuki na Waziri wa Maliasili wa Jamhuri ya Watu wa China, LU Hao wakiwa
katika kikao cha majadiliano baina yao.
|
No comments:
Post a Comment