Na
Asteria Muhozya, Dodoma
Katibu Mkuu wa
Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila amekutana na Ujumbe wa Serikali kutoka nchini India pamoja na
Kampuni ya National India Development Corporation (NMDC) jijini Dodoma, katika
kikao ambacho pia kimeshirikisha watendaji kutoka Wizarani, Taasisi ya Jiolojia
na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) na Tume ya Madini.
Ujumbe huo
umefika wizarani kwa lengo la kuonana na uongozi wa Wizara kwa ajili ya kufanya
majadiliano juu ya nia yao ya kufanya uwekezaji kwenye shughuli za uchimbaji wa
madini na kupata maeneo mapya ya uchimbaji. Awali kampuni hiyo ilikutana na
Shirika la STAMICO na kufanya majadiliano kuona ni kwa namna gani wanaweza
kushirikiana katika utekelezaji wa malengo yao kupitia fursa mbalimbali
zilizopo katika sekta ya madini nchini.
Akizungumza
katika kikao hicho kilichofanyika Desemba 18, Katibu Mkuu Prof. Msanjila amewakaribisha
na kuwapongeza kwa nia yao ya kufanya uwekezaji nchini na kuueleza ujumbe huo
kuwa, kampuni ya NMDC inayo fursa ya kuchagua kuwekeza ikiwa kama kampuni
inayojitegemea ama kwa kuingia ubia na Shirika la Madini la Taifa la (STAMICO).
Aidha, ameuleza
ujumbe huo kuwa, wizara inazo taasisi ambazo zinasimamia masuala yanayohusu
leseni na shughuli za utafiti na kuusisitiza kujadiliana na Kamishna wa Madini,
Mkurugenzi wa Sheria na Tume ya Madini kwa ajili ya kupata taratibu
zinazotakiwa kisheria kuhusu masuala ya leseni na mahitaji mengine wanayotakiwa
kutekeleza kabla ya kuwasilisha mpango huo kwenye ofisi yake. Aidha, aliutaka
ujumbe huo kujadiliana na GST kwa masuala yanayohusu shughuli za utafiti wa
madini.
Pia, Prof.
Msanjila ameishauri kampuni husika kukata leseni ya utafiti kwanza ili kufanya
utafiti katika maeneo waliyoyakatia leseni na kuwasilisha taarifa hizo katika
ofisi ya GST ndipo waendelee na utaratibu wa kupata leseni ya uchimbaji.
Vilevile, ameutaka ujumbe huo kuwa tayari kuwasiliana na wizara pindi unapohitaji
kupata ufafanuzi wa masuala yote ya yanayohusu uwekezaji katika sekta husika.
Kampuni ya NMDC inajishughulisha na shughuli za uchimbaji wa
madini ya chuma na iko chini ya Wizara inayoshughulikia madini ya
chuma ya India. Pia kampuni hiyo pia inajishughulisha na utafiti wa
madini mbalimbali kama vile madini ya chuma, shaba, phosphate, nk.
katika nchi mbalimbali na barani Afrika.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon
Msanjila akieleza jambo katika kikao kati yake na ujumbe wa Serikali ya India
na Kampuni ya National India Development Corporation (NMDC)
|
Sehemu ya ujumbe kutoka Serikali ya India na
Kampuni ya NMDC pamoja na watendaji wa wizara wakifuatilia kikao hicho.
|
Sehemu ya
Watendaji kutoka Tume ya Madini, Taasisi na Jiolojia na Utafiti wa Madini
Tanzania (GST) na Maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia kikao hicho.
|
Katibu Mkuu wa
Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila akiongoza kikao baia yake na ujumbe
kutoka Serikali ya India kilichoshirikisha pia Watendaji kutoka Wizarani, Tume
ya Madini na GST.
|
No comments:
Post a Comment