Na Greyson Mwase,
Dodoma
Leo tarehe 21
Desemba, 2018 Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula ameongoza
kikao cha kazi cha Tume ya Madini kilichofanyika jijini Dodoma. Kikao hicho
kilishirikisha makamishna wa Tume ambao ni Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji
Madini Nchini (FEMATA), Haroun Kinega, Katibu Mkuu
wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Dorothy Mwanyika, Katibu Mkuu wa Wizara
ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Florence Turuka na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt.
Evaristo Longopa.
Wengine ni Dkt. Athanas Macheyeki,
Profesa Abdulkarim Mruma Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani
Manya pamoja na watendaji wa Tume ya Madini.
Pamoja na mambo
mengine kikao hicho kilijadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa majukumu ya
Tume na Mpango Mkakati wa Tume wa miaka mitano (2019/20 -2023/2024). Katika
kikao hicho kati ya masuala yaliyokubaliwa ni pamoja na leseni ambazo
hazifanyiwi kazi kufutwa na tathmini ya kina kufanyika kwa waombaji wa leseni
ili kubaini kama wanakidhi vigezo kama vile uwezo wa kifedha na utaalam.
Kamishna kutoka Tume
ya Madini, Profesa Abdulkarim Mruma (kushoto) akifafanua jambo katika kikao cha
Tume ya Madini kilichofanyika Desemba 21, 2018 jijini Dodoma. Wengine kutoka
kulia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya na
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula.
Kutoka kushoto
makamishna wa Tume ya Madini, Haroun Kinega na Dkt. Athanas Macheyeki
wakifuatilia majadiliano mbalimbali yaliyokuwa yanaendelea katika kikao hicho.
Kutoka kushoto mbele makamishna
wa Tume ya Madini ambao ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
Makazi Dorothy Mwanyika, Naibu
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Evaristo Longopa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa Dkt. Florence Turuka
wakifuatilia ufafanuzi uliokuwa
unatolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula (hayupo
pichani)
Sehemu ya
wajumbe kutoka Tume ya Madini wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yanaendelea
katika kikao hicho.
Mwenyekiti
wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula akifafanua jambo katika kikao hicho
No comments:
Post a Comment