Friday, November 16, 2018

Kamati ya ushiriki wa Watanzania katika sekta ya madini yafanya kikao cha kazi


Na Greyson Mwase,

Leo tarehe 16 Novemba, 2018 Kamati ya Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini  (Local Content) imekutana kwenye Ofisi za Tume ya  Madini zilizopo jijini Dodoma lengo likiwa ni kupokea na kujadili taarifa za kampuni zilizowasilisha mipango  ya ushiriki wa watanzania katika sekta ya madini kama sehemu ya maombi ya leseni za madini.


Mwenyekiti wa Kamati ya Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeki (kulia) akifafanua jambo katika kikao hicho. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya. 

Wajumbe wa Kamati ya Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya (hayupo pichani) katika kikao hicho. 

Sekretarieti ya kikao hicho ikinukuu maelekezo mbalimbali yaliyokuwa yanatolewa na Mwenyekiti wa  Kamati ya Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeki pamoja na wajumbe wengine katika kikao hicho. 

Mwakilishi kutoka Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Ringo Iringo akichangia jambo kwenye kikao hicho. 

Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya akifafanua jambo katika kikao hicho

No comments:

Post a Comment