Monday, October 29, 2018

Ujenzi wa Mgodi wa mfano Lwamgasa wafikia asilimia 80


Na Asteria Muhozya,

Wizara ya Madini imeanza kukutana na Kamati Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuanzia leo tarehe 29 Oktoba hadi Novemba 1, 2018.

Katika kikao cha leo Wizara imewasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.

Akiwasilisha Taarifa kuhusu Ujenzi wa Mgodi wa Mfano wa Lwamgasa,  Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Madini, Augustine Ollal amesema hadi kufikia mwezi Septemba,2018, kazi ya ujenzi wa mgodi na usimikaji wa mitambo ya uchenjuaji imekamilika kwa asilimia 80.

Kuhusu mradi wa One Stop Center, eneo la Mirerani, amesema uko kwenye maandalizi ya kuanza ujenzi  na kuongeza kuwa,   jengo hilo litakapokamilika litakuwa na miundombinu  mbalimbali ikiwemo huduma za Utoaji na Usimamizi wa Leseni za Madini, Uhifadhi wa madini kwa usalama  , Kodi na tozo mbalimbali ikiwemo ofisi za TRA, Huduma za kifedha, ikiwemo Benki na Ofisi za Benki kuu, Hud za tathmini na uthamini madini, Ofisi za Madini na Chumba maalum cha kufanyia minada ya madini.




No comments:

Post a Comment