Monday, October 1, 2018

Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima wakutana kwa ajili ya kujadili taarifa ya uchunguzi wa mfuko wa Trust Fund


Na Greyson Mwase,
Leo tarehe 20 Septemba, 2018 mjini Musoma mkoani Mara, Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima wamekutana na  Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Ulinzi ya Mkoa wa Mara, Watendaji kutoka Wizara ya Madini kwa ajili ya kujadili taarifa iliyowasilishwa na Kamati iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza matumizi ya mfuko wa North Mara Trust Fund kabla ya kutoa maelekezo ya Serikali.


Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima (kulia) wakibadilishana mawazo ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara mara baada ya kuwasili kabla ya kuanza kikao kwa ajili ya kujadili taarifa iliyowasilishwa na kamati iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza matumzi ya fedha katika mfuko wa North Mara Trust Fund.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima (kushoto) akifafanua jambo katika kikao kwa ajili  ya kujadili taarifa iliyowasilishwa na kamati iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza matumzi ya fedha katika mfuko wa North Mara Trust Fund. Kulia ni Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko.


Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima (mbele) wakiahirisha kikao hicho ambapo majadiliano yanatarajiwa kuendelea kesho tarehe 21 Septemba, 2017 kabla ya Serikali kutoa maamuzi yake.

No comments:

Post a Comment