Monday, October 1, 2018

Kairuki afanya mazungumzo na Rais wa FEMATA


Na Nuru Mwasampeta, Dodoma

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki leo tarehe 28 Septemba, 2018, amefanya mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo Nchini (FEMATA), John Bina ambaye aliambatana na Mtendaji Mkuu wa Shirikisho hilo, Bwana Haroun Kinega, ofisini kwake jijini Dodoma.

Katika kikao hicho, Waziri Kairuki amewashukuru wajumbe hao kwa kumtembelea ofisini kwake na kujadiliana masuala mbalimbali katika sekta ya madini kwa lengo la kuboresha utendaji katika sekta ya madini, uchimbaji na wachimbaji wadogo kwa ujumla.

Aidha, Waziri Kairuki amewataka watanzania wenye mawazo chanya ya kukuza sekta ya madini kutosita kufika na kutoa maoni yao ili Serikali iweze kuyafanyia kazi ili kuboresha sekta hiyo kwa manufaa ya jamii nzima ya watanzania na hivyo kuifanya sekta kuchangia zaidi katika pato la taifa, ajira na kukuza uchumi wa nchi.

Akizungumzia lengo la kufika wizarani hapo, Rais wa FEMATA, John Bina amesema ni kujadili kuhusu mafanikio, changamoto, fursa za wachimbaji wadogo zilizopo katika sekta husika pamoja na kujadili namna ya kuendeleza sekta ya uchimbaji mdogo wa madini nchini ikiwa ni pamoja na namna ya kudhibiti utoroshaji wa madini nchini.


Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Shirikisho la Wachimbaji Wadogo wa Madini John W. Bina (Kulia) na kushoto kwa waziri ni Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Wachimbaji wadogo Haroun

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki akipeana mkono na Rais wa Shirikisho la Wachimbaji Wadogo Tanzania (FEMATA) John W. Bina alipomtembelea ofisini kwake.

No comments:

Post a Comment