Monday, August 13, 2018

Waziri Kairuki atembelea eneo la Mpaka wa Namanga


Na Asteria Muhozya,

Waziri wa Madini Angellah Kairuki, akiongozana na Mkuu wa  Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo , Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Longido pamoja na ujumbe aliombata nao wakati wa ziara yake mkoani Arusha, tarehe 9 Agosti,2018, alitembelea eneo la Mpaka wa Namanga, linalotenganisha nchi ya Tanzania na Kenya.

Waziri Kairuki alitembelea eneo husika kwa lengo la kukagua na kuangalia namna shughuli za udhibiti wa utoroshaji wa madini  maeneo ya mipakani  zinavyoendelea.

Waziri Kairuki alisema baada ya kufika eneo husika alikuta kuna suala la changamoto ya upungufu wa wafanyakazi na hivyo kuahidi kulifanyia kazi kwa haraka suala hilo.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alisema changamoto katika eneo hilo ni upungufu wa wafanyakazi na kuongeza kuwa, tayari Waziri wa madini ameahidi kulifanyia kazi suala husika ili kudhibiti utoroshaji madini katika maeneo ya mipaka.

Aliongeza kuwa, tayari Serikali ya Wilaya imeanza kuweka alama kujua mipaka ya Tanzania katika eneo husika ikiwemo kufuatilia njia za panya ambazo zinaweza kutumika kutorosha madini nje ya nchi.

Naye Mkaguzi wa Migodi, Anold Kisheshi alisema kuwa, serikali imekuwa ikitumia njia mbalimbali kudhibiti utoroshaji wa madini katika maeneo ya mipaka.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akimsikiliza Anorld Kisheshi wakati akitoa ufafanuzi wa namna scanner katika eneo hilo zinavyofanya kazi.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akipata maeneo mbalimbali katika eneo Namanga katika mpaka wa Tanzania na Kenya.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akizungumza na wafanyakazi katika kituo cha Namanga katika mpaka wa Tanzania na Kenya wakati alipotembelea kituoni hapo kukagua shughuli za udhibiti wa utoroshaji madini katika maeneo ya mipaka.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akimsikiliza Mkaguzi wa Migodi Ofisi ya Madini Arusha, Anorld Kisheshi (wa pili kushoto) wakati waziri na Ujumbe wake walipotembelea eneo la Namanga kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya ili kuona namna shughuli za uthibiti wa utotoroshaji madini eneo la zinavyofanyika.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akimsikiliza Anorld Kisheshi wakati akitoa ufafanuzi wa namna scanner katika eneo hilo zinavyofanya kazi.

No comments:

Post a Comment