Saturday, August 18, 2018

Serikali yawataka Watanzania kuacha migogoro katika ubia wa uwekezaji


Na Zuena Msuya, Kilimanjaro

Serikali imewataka Watanzania  kuepuka migogoro katika maeno ya migodi hasa inayomilikiwa Kwa ubia na wawekezaji wazawa ili kuondoa taswira mbaya kwa wawekezaji kutoka Matifa mengine yanayokuja nchini kwa lengo la kuwekeza badala yake waungane  kuweka mazingira mazuri na rafiki ya kuvutia wawekezaji hao kuwekeza nchini.

Hayo yameelezwa na Naibu  Waziri wa Madini, Dotto Biteko wakati wa ziara yake mkoani Kilimanjaro  alipotembelea mgodi wa Madini wa Mega unaochimba madini ya shaba .( Mega Copper Company) uliopo katika Kijiji cha Chang`ombe wilayani Mwanga  Mkoani Kilimanjaro, Kwan lengo la kumaliza mgogoro uliopo katika mgodi huo unachimba na kuchenjua madini ya Shaba.

Mgodi huo wa madini ya Shaba unaomilikiwa na Watanzania umekuwa katika migogoro ya kutoelewana wenyewe kwa wenyewe kwa zaidi ya miaka 10 sasa, Licha kumepiga hatau katika uchenjuaji  wa shaba na kwamba hausafirishi madini ghafi nje ya nchi  kama serikali ilivyoagiza.

Kwa mantiki hiyo, Biteko alisisitiza kuwa migogoro haipaswi kupewa nafasi na inarudisha nyuma maendeleo ya watanzania na kuleta taswira mbaya ya Uwekezaji Tanzania katika Mataifa mengine Duniani Kwani kusengskuwa na mgogoro katika mgodi huo wangekuwa wamepiga hatua zaidi kwa manufaa yao na Taifa kwa jumla.

Biteko  alisema “migogoro miongoni ya wabia hasa wazawa haipaswi kufumbiwa macho na mtu yeyote Yule, ambapo alishauri kuwa kama watu, au kikundi wameingia makubaliano ya pamoja katika kuendeleza mgodi au jambo fulani  basi, makubaliano hayo yapelekwe Wizara ya madini  au katika mamlaka husika yasajiliwe kuepusha migogoro.

Aidha aliweka wazi kuwa kutokana na mgogoro, Serikali imetoa Miezi 3 kwa mgodi huo kumaliza tofauti zao na kuendelea na shughuli za uzalishaji, na endapo watashindwa kufanya hivyo, itawaandikia hati ya makosa na kisha kuwanyang'a mgodi huo na kuwapa watu wengine.

“Ninyi wote ni Watanzania tena ni ndugu kwa nini mnagombana? , Mnakuja kuwa Sheria ya madini inaruhusu kuwafungulia hati ya mashitaka na kuwafutia leseni endapo mgogoro huo  hautakwisha na utakuwa na  viashiria vya uvunjivu wa amani na Mkishindwa kuumaliza ndani ya muda uliotolewa Serikali unaingia Kati na kufanya maamuzi,  nawakumbusha  watanzania wote  hasa wanaoishi katika maeneo karibu na migodi kuepuka migogoro ili sekta ya mdini iendeleee kuimarika” alisisitiza Naibu waziri Biteko.

Vilevile alitoa  wito kwa wanatanzania wenye uwezo wa kuongeza thamani  ya madini wafanye hivyo ili kuongeza pato la taifa na mwananchi mmoja mmoja  kuliko kusafirisha  madini ghafi  nje ya nchi kwa kuwa faida kubwa zinapata nchi zinazo nunua madini ghafi hayo na kuyaongeza thamani.

Kwa mujibu wa Naibu waziri Biteko  mgogoro ulipo katika mgodi huo kati ya  wabia Watanzania wawili ambao kila mmoja alikuwa na mbao wake kutoka nje, ambao waliingia  makubaliano  ya kuanzisha mradi huo ndani ya miezi sita,  baadae Kuliitokea kutoelewana na kUsababisha   mmoja kati yao kuanza uzalishaji  kabla ya kumshirikisha mwenzie.

Mmoja wa wabia hao ni Ally Nyanza kutoka ambaye  alisema kuwa mgodi huo una ukubwa wa heka 25, ambapo  kwa sasa  wapo kwenye majaribio ya kuchimba na kuchenjua shaba Ambapo wanauwezo wa kuzalisha tani 8-10 za shaba kwa siku.  

Alisema Bado wanaendelea na tafiti huku wakiendelea na uzalishaji, soko kubwa la shaba hiyo  liko nchini  China na kutokana na tafiti hizo wamegundua eneo hilo lina  chokaa ambayo hutumika kwenye uzalishaji wa saruji.

Nyanza alismea changamoto kubwa ilikuwa na mgogoro kati yao na uliosabababisha kusimamisha uzalishaji kwa muda mrefu, kwa sasa wanafuata maelekezo ya Naibu waziri kupata muafaka wa kufanya kazi pamoja.

Naye Nassib  Mfinanga  alisema   wamemeridhika na maamuzi ya Naibu Waziri wa Madini na kwamba watakaa kama familia ili tusonge  mbele kwani mgogoro huo umekuwa ukituchelewesha na kutupa hofu kuwekeza bila kuwa na usalama, jambo hili lilikuwa ngumu kwetu.

Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Aaron Mbogho alisema uwepo wa mgodi huo ni chachu ya maendeleo katika wilaya hiyo tunasuburi wameanza uzalishaji pamoja wazingatie sheriana kanuni za wizara  serikali bado inatamani kuona watoka kwenye uongezajiwathani ya shaba 90% hadi kufikia 100%.


Naibu Waziri  wa madini, Dotto Biteko, akizungumza na akina mama wanaofanya kazi katika mgodi wa shaba wa Mega. 

Naibu waziri wa madini, Dotto Biteko (kulia) akipita katikati ya Mbale za shaba zilizoandaliwa tayari kwa kuchenjuliwa. 

Sehemu ya mtambo unaotumika Kuchenjua shaba. 

No comments:

Post a Comment