Na Zuena Msuya, Mheza Tanga
Serikali imesema
itawaleta wataalam kutoka kituo cha Utafiti wa Miamba(GST), Wizara ya Maliasili na Mazingira kwenye eneo walilokuwa
wakitumia wachimbaji wadogo kwa shughuli za madini, ambalo pia linadaiwa kuwa
liko katika chanzo cha maji, kufanya utafiti na kujiridhisha kama eneo hilo
liruhusiwe kuendeleza na shughuli za uchimbaji madini ama laa.
Hayo
yalisemwa na Naibu waziri wa Madini Dotto Biteko alipotembelea katika kijiji
cha Sakale katika Kata ya Mbomole Tarafa ya Amani wilayani Mheza mkoani Tanga, wakati
akizungumza na wananchi waliomuelezea kero yao ya kuzuiwa na serikali
kutokuchimba madini eneo hilo licha ya kuwatokuwepo na viashiria vya uharibifu wa
mazingira na misitu kama serikali inavyosema.
Naibu
Waziri Biteko, alisema kuwa kiu ya serikali ni kuwapatia maeneo ya uchimbaji
wachimbaji wadogowadogo ili waweze kubadilisha maisha yao kupitia uchumi wa
madini, hii ni kutokana Rais kubadilisha sheria za nchi kwa upande wa madini
kutoka kuwanufaisha wageni na sasa kuwanufaisha watanzania.
“Serikali
yenu ni sikivu,Mheshimiwa Rais amebadilisha sheria ya madini ili kuwanufaisha
watanzania badala ya wageni ,hapa leo tumekuja kuangalia kwa macho ili tufanye uamuzi
sahihi …siwezi kumiambia mchimbe sasa hivi ila tutaleta wataalamu wetu wa
GST,maliasili na mazingira kwa pamoja ili waje kuona uwezekano wa kupewa eneo
la kuchimba ikiwa hapa au kwengine”alisema.
Aidha
aliongeza kuwa wananchi lazima wafundishwe kufuata sheria za madini haswa
katika kuhama matumizi ya
zebaki katika kuchenjua madini ambayo yana athari kubwa kwenye mazingira na
miili ya binadamu kutumia madini ya Sayayi ambayo hayana madhara.
Kwa
upande wa wananchi wa eneo hilo, walimueleza naibu waziri huyo kuwa madini
katika eneo hilo yaligunduliwa mwaka 2013 na yanapatikana kwenye miamba na siyo
kwenye chanzo cha mto kama serikali inavyosema lakini walizuiwa kwa tahadhari
ya uharibifu wa mazingira na misitu ya asili.
Walisema
kuwa kutoka uliopo mwamba unaosadikiwa kuwa na madini na chanzo cha maji ni
zaidi ya mita sitini na ilipo hifadhi ya msitu wa asili wa Amani ni zaidi ya
mita 3,000 lakini wamekuwa wavumilivu kusubiri hatima ya serikali.
“Mheshimiwa
Naibu Waziri uchumi tunao lakini tunakufa maskini…hapa madini yapo lakini
serikali imetuzuia kwa hatari ya uharibifu wa mazingira ..sisi tunakuhakikishia
hakuna uharibifu wowote wa mazingira utakaotokea,”
alisema Shetwai.
Naye
diwani wa kata hiyo Anord Mlowe alisema kuwa wataalamu walikuja kupima mwamba na baadae ukaanza kutoa madini lakini
baadae kukaanza mabishano kati ya watu wa maliasili,maji na mazingira kuhusu
usafishaji wa madini kwa kutumia zebaki lakini mkuu wa wilaya ya Muheza aliyepita Subira Mgalu
alijiridhisha kuwa hakuna madhara lakini serikali ikaweka zuio.
Alimuomba
waziri kuwaruhusu ili waweze kuchimba kutoka maeneo yalipo mmwamaba wa madini
ni mashamba ya wananchi na sio eneo la hifadhi kutokana wameyarithi kutoka kwa
mababu
zao.
Akizungumzia
eneo hilo, mbunge wa jimbo la Muheza, Balozi
Adadi Rajabu alimuomba Naibu Waziri , Biteko kuleta wataalamu wa madini kuja
kupima ili kuona kama madini hayo yanatoka milimani au yapo kwenye mto ili
kuona namna ya kuwasaidia kupewa eneo la uchimbaji.
“Mheshimiwa
naibu waziri pale mwamba uko pembeni kutoka chanzo cha maji na wananchi wa
Sakale kata ya Mbomole wametunza msitu wa asili wa Amani….hivyo wakipewa eneo
la uchimbaji wataweza kutunza msitu bila ya kuathiri chanzo cha maji” alisema.
Awali
Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mhandisi Mwanaasha Tumbo akisoma taarifa ya zuio la
uchimbaji wa madini eneo hilo, alisema lengo ni kulinda mazingira na chanzo cha
maji licha ya sheria katika maeneo hayo matatu ya madini, mazingira na
maliasili kukinzana jambo ambalo linaleta ugumu kwa watendaji kuwadhibiti
wachimbaji hao.
![]() |
Naibu
Waziri wa Madini, Dotto Biteko, (mwenye Tshit nyekundu) na Mbunge wa Mheza
Balozi Rajab Adad (mbele) wakielekea eneo lililokuwa likitumiwa na wachimbaji
wadogo kuchimba madini pia likidaiwa kuwa chanzo cha maji katika hifadhi ya
misitu wa asili wa amani, mheza Tanga.
![]() |
Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko,( katikati) akizungumza na
wananchi wa Kijiji cha Sakale, Mheza mkoani Tanga, waliokuwa wakiomba
kuruhusiwa kufanya shughuli za uchimbaji madini katika eneo linalodaiwa kuwa ni
chanzo cha maji yanayotumika Mkoa wa Tanga.
No comments:
Post a Comment