Na
Zuena Msuya, Tanga
Serikali imeiagiza
Tume ya Madini Tanzania, kutoa hati ya makosa kwa Kampuni ya Canaco inayomiliki
leseni ya Uchimbaji Madini wa Kati iliyopo
katika Kijiji cha Magambazi Wilayani Handeni Mkoani Tanga, na kuzuia mali na
mitambo yote iliyopo eneo hilo kutokana kukiuka masharti ya leseni hiyo ya
uchimbaji madini ya dhahabu na kwenda kinyume na Sheria ya Madini yam waka 2010
na marekebisho yake ya mwaka 2017 pamoja na kanuni za mwaka 2018.
Agizo hilo limetolewa
na Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko, wakati wa ziara yake ya kukagua
shughuli za uchimbaji madini katika Wilaya ya Handeni mkoani Tanga, ambapo
pamoja na mambo mengine pia aliagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(Takukuru) kufanya uchunguzi katika sakata la utoroshwaji wa Carbon zenye madini ambazo ziliibwa
usiku kutoka eneo hilo na kupelekwa mkoani Mwanza kwa ajili ya kuyeyushwa ili
kupata dhahabu kinyume cha utaratibu.
Waziri Biteko alisema
kuwa mwekezaji huyo awali alifika katika Wizara ya Madini na kuomba kibali cha
kusafirisha carbon tani 2.23 kwenda
mkoani Mwanza katika kiwanda cha JEMA AFRICA LTD kwa ajili ya kuchenjuliwa lakini wakanyimwa
kutokana na matatizo yao ya ndani lakini
baadae wakachukua kibali cha kughushi kutoka Dodoma kwa ajili ya kusafirishia carbon kupeleka Mwanza.
Hawa watu walikuja
ofisini ya madini Handeni kuomba kibali
cha kusafirisha carbon tani 2.23 kwenda
Mwanza kwa ajili ya kuchenjuliwa lakini walinyimwa kutokana na sababu zao za
ndani zilikuwepo muombaji kutokuwa mmiliki wa leseni ya Canaco lakini cha
kushangaza walitorosha carbon tani 2.23
usiku wa manane na kwenda kuchukua kibali cha kughushi kutoka
ofisi ya madini Dodoma kinachoonesha carbon tani 1.5 tualisema.
Aliongeza Baada ya
kuichakata carbon tani 1.5 Mwanza kiasi
kingine hakijulikani kilipo mpaka sasa haiwezekani jambo hili lichukue muda
katika uchunguzi nakuagiza OCD kadri utakavyoona katika harakati zako za
kiuchunguzi hawa watu wakamatwe na nawaomba TAKUKURU nao watusaidie katika
kuchunguza wa jambo hili alisema.
Mbali na hivyo pia
aliumuelekeza Kamishna wa Tume ya Madini Dkt.Athanas Macheyeka kumpa mwekezaji
huyo hati ya makosa (default notice)
kwa ajili ya kurekebisha makosa waliyonayo kwenye leseni ya uchimbaji wa madini
na kama watashindwa kurekebisha makosa
kwa muda uliotajwa na sheria, leseni yao ifutwe wapewe wawekezaji wengine walio
makini.
Sheria ya madini
inamtaka mwenye leseni ya madini achimbe siyo atumie mabaki yaliyochimbwa na
wachimbaji wengine ayachenjue
kamishna wa tume ya madini kati ya leo na kesho
wape default notice kwa ajili ya
kurekebisha makosa yao na wasipo rekebisha leseni yao ifutwe watafutwe
wawekezaji wengine serious alisema.
Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin
Gondwe alimuhakikishia Naibu Waziri kutekeleza maagizo aliyoyatoa kwa
kuwachukulia hatua kali wawekezaji hao ikiwemo
kuwakamata wahusika.
Alisema kuwa awali
baada ya kubaini wizi katika mgodi huo aliunda kamati ya ulinzi na usalama
iliyohusisha Afisa madini mkazi,Afisa maendeleo,Afisa misitu na Afisa
usalama ambapo baada ya uchunguzi kwenye mgodi ,maabara ,makontena pamoja na kwenda
kwenye maabara za madini Dodoma,Bahi na Mwanza walibaini carbon hiyo iliibwa na kupelekwa
kwatika kiwanda hicho cha JEMA AFRICA LTD.
Katika taarifa ya
kamati ya maalum iliyoundwa na Wilaya ya Handeni kufuatia maelekezo ya Naibu
Waziri Biteko alipotembelea mgodi huo mapema mwaka huu ilibaini
makosa tisa ambayo ni
ukiukwaji wa sheria,kanuni na utaratibu
wa kuingia mkataba usiotambulika kisheria kati ya kampuni ya CANACO na TANZANIA
GOLD FIELDS,mgodi kutoendelezwa kwa muda uliopangwa kisheria ndani ya miezi
18,kuchenjua madini bila leseni na utumiaji wa kemikali ya Sayanaidi bila ya
kibali cha mkemia mkuu wa serikaiai.
Mambo mengine ni
kuwepo kwa udanganyifu wa kampuni ya CANACO na TANZANIA GOLD FIELDS kwa kudai
kuwapo katika hatua ya majaribio wakati kuna usimikaji wa mitambo ya uchenjuaji
bila kibali cha mkaguzi mkuu wa mgodi,kuendesha shughuli za mgodi bila kuwepo
na meneja aliyeteuliwa kisheria,kufanya uchenjuaji wa madini na marudio ya uchimbaji unaosababisha
uharibifu wa mazingira bila ya kuwa na vibali vinavyostahiki,kusimika mtambo wa
uchenjuaji wa marudio bila ya kuwa na vibali vya mkaguzi mkuu wa mgodi.
![]() |
Naibu Waziri,Dotto
Biteko (kulia),Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe (Katikati)wakikagua eneo
la mgodi wa Madini, katika kijiji cha Magambazi wilayani Handeni mkoani Tanga.
|
No comments:
Post a Comment