Wednesday, June 13, 2018

Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amezindua Maabara kubwa na ya kisasa Afrika na ya pili Duniani kwa upimaji wa madini


Na Zuena Msuya, Dar es Salaam

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kasim Majaliwa amezindua Maabara ya kisasa ya utambuzi wa uasili wa madini iliyojengwa katika Kituo cha Madini na Jiosayansi Afrika kilichopo eneo la Kunduchi Mtongani, jijini Dar es salaam.

Akizungumza mara baada ya kuzindua maabara hiyo, Juni 8, 2018, Waziri Mkuu Majaliwa alisema maabara hiyo itakuwa na uwezo wa kutambua asili ya madini yote yanayochimbwa NA kupatikana duniani.

Vile vile italinda madini ya kila nchi husika hasa kwa nchi za Afrika na kumaliza kabisa tatizo la utoroshwaji wa madini ya aina yoyote kutoka nchi moja kwenda nyingine.

“Maabara hiyo itakuwa na uwezo wa kutambua mahali ambapo madini hayo yamechimbwa au yanapatikana, na haitakuwa  rahisi kwa mtu yeyote kufanya udanganyifu wa kutorosha madini hayo kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwani kila nchi yatakapokuwa yatakapopelekwa madini hayo vipimo vitaonyesha asili yanapotoka madini hayo”, alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Alifafanua zaidi kuwa Maabara hiyo pia inauwezo mkubwa wa kupima na kutambua asili ya madini Bati( Tin),Tantalam na Tantalite, yanapochimbwa na yanapotoka, jambo ambapo litaondoka tatizo la kubaini kuwa madini hayo lilipo sasa kwa nchi za afrika zinazochimba madini hayo ikiwemo Burundi, Rwanda, Uganda na Jamhuri ya Kidemograsia ya Congo.

Hivyo amezishauri nchi za Afrika kutumia maadara hiyo ambayo kwa sasa inapatikana Tanzania pekee kwa nchi za afrika na niya pili kujengwa duniani, ili nchi hizo ziweze kufahamu madini yake halisi yanayopatikana katika nchi husika.

“ kwa mfano hapa Tanzania tunawachimbaji wadogo wengi sana wanachimba madini lakini wengi wao wanashindwa kutambua ni madini gani wanachimba, pia tunapokamata madini mipakani wengi husema madini hayo yanatoka nchi jirani na hivyo tunakosa uthibitisho, sasa maabara hii ni muarobaini wa kutatua changamoto zote hizi, na ni imani yangu kubwa italeta manufaa makubwa katika sekta ya madini”, alisisitiza Waziri Mkuu Majaliwa.

Aliweka wazi kuwa kuwepo kwa maabara hiyo Afrika kutamaliza kabisa tatizo la uotoshwaji wa madini kutoka sehemu moja kwenda nyinge na kuondoa udanganyifu na unaofanywa na baadhi ya watu wasio waaminifu kwa kusema ukweli kuhusu mahali yanapopatikana madini husika.

Maabara hiyo inauwezo mkubwa wa kupima madini na kutumia muda mfupi katika kutambua uhalisia wa madini.

Sambamba na hilo, Waziri Mkuu, Majaliwa alisema maabara hiyo ya kisasa itarahisisha biashara ya madini kwa kila nchi husika na kuleta manufaa zaidi kwa taifa na wake.


Waziri Mkuu Kasim Majaliwa (kushoto) akilakiwa na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Kituo cha Madini na Jiosayansi Afrika kuzindua Maabara ya kwanza ya kisasa Afrika na ya pili duniani ya kutambua uasili wa madini.


Waziri Mkuu Kasim Majaliwa (kushoto) akisalimiana na Naibu wa Waziri wa Madini, Stansilaus Nyongo mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Kituo cha Madini na Jiosayansi Afrika alipowasili kuzindua Maabara ya kisasa Afrika na ya pili duniani ya kutambua uasili wa madini.


Waziri Mkuu Kasim Majaliwa( kushoto) akisalimiana na Naibu wa Waziri wa Madini, Dotto Biteko mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Kituo cha Madini na Jiosayansi Afrika alipowasili kuzindua Maabara ya kisasa Afrika na ya pili duniani ya kutambua uasili wa madini.


Waziri Mkuu Kasim Majaliwa( kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila,(kulia) mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Kituo cha Madini na Jiosayansi Afrika alipowasili kuzindua Maabara ya kwanza ya kisasa Afrika na ya pili duniani ya kutambua uasili wa madini.


Waziri Mkuu Kasim Majaliwa (kulia) akipata maelezo  ya namna maabara hiyo inavyofanya kazi kutoka kwa mmoja wa wakufunzi   katika Kituo cha Madini na Jiosayansi Afrika kuzindua Maabara ya kwanza ya kisasa Afrika na ya pili duniani ya kutambua uasili wa madini,

Waziri Mkuu Kasim Majaliwa (kushoto) akipeana mkono na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki mara baada ya kufungua kitambaa kuzindua  Maabara ya kwanza ya kisasa Afrika na ya pili duniani ya kutambua uasili wa madini.

No comments:

Post a Comment