Thursday, June 7, 2018

Kikao cha 21 cha Makatibu Wakuu wa Kituo cha AMGC chafanyika Tanzania


Na Rhoda James, Dar es Salaam

Makatibu Wakuu kutoka nchi Wanachama wa Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC) wameshiriki katika kikao cha 21 cha Kituo hicho kilichopo Kunduchi, jijini Dar es Salaam.

Akifungua rasmi kikao hicho kilichofanyika tarehe 6-7 Juni, 2018, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Tanzania, Prof. Simon Msanjila ambaye anashiriki kwa mara ya kwanza, alisema kuwa, kituo hicho hakina budi kuweka jitihada katika kuhamasisha nchi  nyingine za Afrika ambazo bado hazijajiunga ili ziweze  kujiunga  na kituo hicho.

Pia, alieleza kuhusu umuhimu wa kituo kuendelea kuweka msisito kwa nchi wanachama kulipa ada za uanachama kwa wakati na kuhakikisha kuwa kinatekeleza majukumu yake kwa ubora uliokusudiwa.

Akichangi mada, Prof. Msajila alizungumzia kuhusu suala la upatikanaji wa eneo la ujenzi wa vinu vya kuchenjua na kuongeza thamani madini na kushauri kuhusu kuzingatia suala ya uhifadhi wa mazingira.

Pia, Profesa Msajila alikitaarifu kikao hicho kuhusu ushiriki wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Dkt. Tito Mwinuka na Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Amon Maganga pamoja na Wataalam mbalimbali kutoka taasisi hizo  katika Mkutano wa 38 wa Wakuu wa nchi wanachama utakaofanyika tarehe 8 Juni, 2018.

“Nimeeleza kuhusu ushiriki wa Watendaji hao kwa lengo la kujadili suala la kufanya biashara na kituo cha AMGC kwa kuwa vipo vifaa ambavyo kituo chetu kinaweza kuvizalisha kwa matumizi ya taasisi za REA na TANESCO,” alisema Prof. Msanjila.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kikao hicho Dkt. Kojo Busia alisema kuwa, asilimia 75 ya madini ya Coltan hupita katika Bandari ya Dar es Salaam Tanzania kuelekea nchi jirani ukilinganisha na asilimia 25 ambayo hupita Mombasa nchini Kenya na kueleza umuhimu kituo hicho kuboreshwa ili kutoa huduma bora zaidi.

Pia, Dkt. Busia alisisitiza suala la kituo cha AMGC kuona namna bora ya kuungana na Taasisi ya African Minerals Development (AMDC) ili kuwa chombo kimoja ambalo litapelekea kuongeza ufanisi wa kituo hicho.

Nchi wanachama wa kituo cha AMGC ni Tanzania, Angola, Msumbiji, Sudani Kaskazini, Ethiopia, Uganda, Kenya, Comoro na Burundi.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msajila akichangia mada katika kikao cha 21 cha Makatibu wakuu kilichofanyika katika Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC) Kunduchi, jijini Dar es Salaam. 


Wajumbe mbalimbali waliohudhuria kikao cha 21 cha Makatibu wakuu kilichofanyika katika Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC) Kunduchi, jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Bodi wa Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC), Assa Mwakilembe akichangia mada katika kikao hicho. Kulia kulia kwake Mjumbe kutoka nchi ya Uganda.


Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya akichangia mada katika kikao cha 21 cha Makatibu Wakuu kilichofanyika katika Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC) Kuduchi, jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Kikao cha 21 cha Makatibu Wakuu Dkt. Kojo Busia akichangia mada katika kikao cha 21 cha Makatibu Wakuu kilichofanyika katika Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC) Kuduchi, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Madini, Profesa Simon Msajila na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC) Ibrahim Shadard.


Wajumbe mbalimbali waliohudhuria kikao cha 21 cha Makatibu wakuu kilichofanyika katika Kituo cha Madini na Jiosayansi cha Afrika (AMGC) Kunduchi, jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment