Thursday, May 24, 2018

Wizara ya Madini yafanya semina ya mabadiliko ya sheria ya madini kwa Kamati za Bunge


Na Samwel Mtuwa, Dodoma

Wizara ya Madini imefanya Semina kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini pamoja na Kamati ndogo ya Sheria ya Bunge juu ya Mabadiliko ya  Sheria ya Madini ya Mwaka 2010.

Akizungumza katika semina hiyo, Katibu wa Tume ya Marekebisho ya Sheria Tanzania, Casmir Kyuki, alieleza kuwa, semina hiyo imelenga kuwaelemisha Wabunge  kuhusu   Sheria  Mpya ya Madini ya mwaka 2017 baada ya kufanyika Marekebisho kadhaa katika Sheria ya Madini ya Mwaka 2010.

Aidha, pamoja na kupata elimu kuhusu sheria hiyo, wajumbe  wa kamati hizo walipata fursa ya  kuelimishwa kuhusu  Kanuni Saba za  Sheria ya Madini ambazo ni Kanuni ya Umiliki wa madini; Kanuni ya Biashara ya madini; Kanuni ya uendeshaji wa wananchi Kanuni ya madini ya mionzi.

Kanuni  nyingine ni pamoja na Kanuni ya uongezaji thamani madini na Kanuni ya utafiti wa kijiolojia  na Kanuni ya hifadhi ya ukaguzi wa hesabu na kumbukumbu.

Kwa upande wake, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Flurence Luoga aliwaeleza wabunge  kuhusu sababu za maboresho  ya Sheria ya Madini ya  Mwaka 2010,  Sheria ilimpa mwekezaji uhuru mkubwa  ndani ya sekta ya madini.

"Uhuru huo ni  pamoja na uhuru wa kuchimba , kusafirisha , kufanya uchenjuaji nje ya nchi, pamoja na  kufanya tafiti bila kuwasilisha taarifa  za kijiolojia na madini,"alieleza Luoga.

Akielezea juu ya sababu za kuwepo kwa uhuru huo katika sekta ya madini kabla ya maboresho ya Sheria ya 2018, Gavana  Luoga alifafanua kuwa suala hilo lilitokana na Sheria zilizokuwepo tangu enzi za Serikali ya kikoloni.

Semina hiyo iliendeshwa na wabobezi  wa masuala ya sheria , fedha na madini ambapo walitoa mada mbalimbali  kuanzia  historia ya mikataba ya kisheria ya kitaifa na kimataifa juu ya sekta ya madini tangu enzi za serikali za kikoloni za Ujerumani na Uingereza.

Watoa mada Wakuu katika semina hii walikuwa  Mkurugenzi Mkuu wa  Taasisi ya Jiolojia na Utafiti Madini Tanzania (GST), Profesa Abdulakarim Mruma Profesa Gavana wa  Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Florence Luoga na   Katibu wa Tume ya kurekebisha sheria Tanzania Casmir Kyuki.

Semina ilifanyika tarehe 19 Mei 2018, katika ofisi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndani ya ukumbi mdogo wa Pius Msekwa  na kuhudhuria na  kutoka Vyama mbalimbali vya siasa, Watendaji wa Wizara na Watalaam wa  Sheria na Madini  kutoka wizara ya  Madini.

Baadhi ya Wabunge  na Watendaji wa Wizara wakifuatilia semina  kuhusu Sheri ya Madini ya Mwaka 2017.
Baadhi ya Wabunge  na Watendaji wa Wizara wakifuatilia semina  kuhusu Sheri ya Madini ya Mwaka 2017.


Baadhi ya Wabunge  na Watendaji wa Wizara wakifuatilia semina  kuhusu Sheri ya Madini ya Mwaka 2017.

Baadhi ya Wabunge  na Watendaji wa Wizara wakifuatilia semina  kuhusu Sheri ya Madini ya Mwaka 2017.

Baadhi ya Wabunge  na Watendaji wa Wizara wakifuatilia semina  kuhusu Sheri ya Madini ya Mwaka 2017.

Baadhi ya Wabunge  na Watendaji wa Wizara wakifuatilia semina  kuhusu Sheri ya Madini ya Mwaka 2017.

No comments:

Post a Comment