Friday, May 11, 2018

Waziri Kairuki akutana na Balozi wa Japan nchini


Na Samwel Mtuwa, Dodoma

Waziri wa Madini,  Angellah Kairuki leo amekutana na  balozi wa Japani nchini, Masaharu Yoshida mjini  Dodoma lengo likiwa ni kujadiliana namna ya kushirikiana kwenye uwekezaji wa madini nchini.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Kairuki alisema lengo la kikao hicho lilikuwa ni kujadili maandalizi ya Jukwaa la Uwekezaji  katika Sekta ya Madini kati ya  Tanzania na  Japan.

Alisema kupitia jukwa hilo, wadau kutoka nchi zote mbili watafahamu  fursa za uwekezaji  katika sekta ya madini kama vile uongezaji  thamani ya madini yapatikanayo nchini na namna ya kuwajengea uwezo wachimbaji wadogo.

Kairuki aliongeza kuwa mbali na fursa mbalimbali katika sekta ya madini jukwaa hilo litaangalia namna ya kuongeza ajira kwenye sekta hiyo kwa kuwajengea uwezo wadau wa madini nchini.

Balozi Yoshida aliambatana na Mkurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya uwekezaji katika sekta  ya madini.


Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kushoto) akibadilishana mawazo na Balozi wa Japan Nchini Masaharu Yoshida (kulia) ofisini kwake mjini Dodoma mapema leo tarehe 09 Mei, 2018.


Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kushoto) akiagana na Balozi wa Japan Nchini Masaharu Yoshida (kulia) mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho.


Waziri wa Madini,  Angellah Kairuki (wa pili kutoka kulia) na Balozi wa Japan Nchini Masaharu Yoshida ( wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa  Japan mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho.

No comments:

Post a Comment