Tuesday, May 8, 2018

Naibu Waziri Nyongo afunga mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Madini


Na Greyson Mwase,

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amefunga mkutano wa kwanza wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini uliofanyika mjini Morogoro leo tarehe 07 Mei, 2017.

Akifunga baraza hilo, amesema sekta ya madini ni muhimu katika kuinua uchumi wa nchi na kuwataka watumishi kutoa kipaumbele kwenye uwekezaji wa viwanda vya kuongeza thamani madini nchini.

Naibu Waziri Nyongo amewataka watumishi kuzingatia sheria na kanuni za utumishi wa umma ili kuleta tija kwenye utendaji kazi.

Aidha, amewataka wajumbe wa baraza na watumishi kwa ujumla kutekeleza maazimio waliyojiwekea katika mkutano huo ili kuboresha utendaji kazi wa Wizara na kuleta matokeo chanya katika Sekta ya Madini.

Miongoni mwa maazimio yaliyofikiwa katika mkutano huo ni pamoja na  wachimbaji wadogo wa madini wawezeshwe kwa kuwekewa mazingira mazuri ya utendaji kazi, taasisi zote zilizopo chini ya Wizara ziunde mabaraza na  watumishi wote ambao hawajajaza fomu za maadili watekeleze wajibu huo.

Kikao kingine cha baraza hilo kimependekezwa kufanyika mjini Morogoro baada ya mwaka mpya  wa fedha 2018/2019.


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akifunga mkutano wa kwanza wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini uliofanyika mjini Morogoro leo tarehe 07 Mei, 2017. 


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati waliokaa mbele), Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Simon Msanjila ( wa nne kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na menejimenti ya  Wizara ya Madini.


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati waliokaa mbele), Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Simon Msanjila ( wa nne kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) Tawi la Wizara ya Madini.


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati waliokaa mbele), Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Simon Msanjila ( wa nne kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini.


Kutoka kulia Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa RasilimaliWatu kutoka Wizara ya Madini, Issa Nchasi, Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Simon Msanjila na Katibu wa TUGHE mkoa wa Dodoma, Mchenya John wakiwa katika picha ya pamoja.


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati waliokaa mbele), Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Simon Msanjila ( wa nne kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na madereva wa wizara hiyo mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo.

No comments:

Post a Comment