Friday, January 19, 2018

Naibu Waziri Nyongo afanya ziara Maswa–Simiyu

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) akisalimiana na wakazi wa Kata  ya Mbalagane iliyopo katika wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, mara baada ya kuwasili ili kukusanya kero zao kupitia mkutano wa hadhara.
Sehemu ya umati wa wakazi wa Kata ya Mbalagane iliyopo katika wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, wakisikiliza ufafanuzi wa kero zao kutoka kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara.
Mkazi wa Kata  ya Mbalagane iliyopo katika wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, Pulwa Sungwa akiwasilisha kero yake kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara.

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo leo  tarehe 29 Oktoba, 2017 amefanya ziara ya  kikazi katika wilaya ya Maswa mkoani Simiyu lengo likiwa ni kukutana na  wananchi na kukusanya kero mbalimbali hususan katika masuala ya madini. Katika ziara hiyo  aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Seif Shekalaghe pamoja na wataalam kutoka halmashauri. Ziara hii ni mwendelezo wa ziara aliyoifanya katika mikoa ya  Kagera na Geita kwa ajili ya kufahamu shughuli za migodi ya serikali, binafsi na wachimbaji wadogo.

No comments:

Post a Comment