Wednesday, November 22, 2017

Takukuru kuhakiki matumizi STAMIGOLD – Kairuki

Uchimbaji wa madini ya dhahabu ukiendelea katika moja ya mashimo  yanayomilikiwa na Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo mkoani Kagera. 

 Kaimu Meneja Uchimbaji kutoka Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo, Rashil Rulanga (kulia mbele) akielezea shughuli za uchimbaji zinavyofanyika katika mgodi huo kwa Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kushoto mbele) mara alipofanya ziara katika mgodi huo tarehe 27 Oktoba, 2017. Wa pili kushoto mbele ni Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo. 

 Shughuli za utafiti wa madini ya dhahabu zikiendelea katika Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo uliopo mkoani Kagera.

 Kutoka kushoto mbele ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Balozi Alexander Muganda,   Waziri wa Madini, Angellah Kairuki, Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo na Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo, Saada Malunde wakiendelea na ziara katika eneo la Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo. 

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (katikati) akitoa maelekezo kwa Kaimu Meneja Uchenjuaji kutoka Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo, Joseph Kamishina (kulia mbele) katika ziara hiyo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo.

 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kushoto) akifafanua jambo katika ziara hiyo.


Kaimu Meneja Uchenjuaji kutoka Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo, Joseph Kamishina (katikati mbele) akimwongoza Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ( wa pili kulia) na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa tatu kulia) kuelekea kwenye eneo la uchenjuaji katika mgodi huo. 

 Kaimu Meneja Uchenjuaji kutoka Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo, Joseph Kamishina(katikati) akielezea shughuli za uchenjuaji madini zinavyofanyika kwa Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kushoto) katika ziara hiyo. Kulia ni Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo

Mmoja wa wafanyakazi katika Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo, Sara Mkama akiwasilisha  kero yake kwa Waziri wa Madini, Angellah Kairuki na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ( hawapo pichani) mara Mawaziri hao walipokutana na watumishi wa mgodi huo kwenye ziara hiyo lengo likiwa ni kusikiliza na kutatua kero zao.

Sehemu ya watumishi wa Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo, wakisikiliza maelezo  yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (hayupo pichani)

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kushoto) na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) wakisikiliza kero mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa na watumishi mbalimbali wa Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo (hawapo pichani)
 
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ameitaka Bodi ya  Wakurugenzi wa Shirika la  Madini la Taifa (STAMICO) kuwasilisha  taarifa zote za gharama za uendeshaji wa Mgodi wa Uchimbaji Dhahabu  wa STAMIGOLD – Biharamulo  ili  kujiridhisha  pamoja na kuchukua hatua za kisheria iwapo kama kuna taratibu za manunuzi zimekiukwa.

Kairuki ameyasema hayo leo  tarehe 27 Oktoba, 2017 alipofanya ziara katika mgodi huo uliopo wilayani Biharamulo mkoani Kagera lengo likiwa ni kufahamu shughuli za migodi ya serikali, binafsi na wachimbaji wadogo.

Alisema kuwa gharama  za uendeshaji wa shughuli za mgodi  huo zimekuwa ni kubwa mno pamoja na madeni hali inayopelekea shirika hilo  kujiendesha kwa  hasara badala ya kujiendesha kwa faida.
Aliendelea kusema kuwa STAMIGOLD  imekuwa ikitumia  gharama kubwa sana katika uendeshaji wa shughuli zake kwa kutumia mashine za kukodi na kutaka watendaji wa mgodi huo kuwa wabunifu  kwa kuibua mikakati mipya kupunguza matumizi na kuzalisha  faida kubwa ili  hatimaye waweze kutumia vifaa vyake badala ya kukodi.

“ Ukiangalia  gharama inayotumika kukodi mashine  za uchorongaji  na uchimbaji madini na nyinginezo utabaini kubwa sana ambapo kama STAMIGOLD ingejipanga ingekuwa na uwezo kabisa wa kununa mashine na mitambo yake yenyewe na kuepuka gharama kubwa za kukodi.
Aidha, Waziri Kairuki alielekeza Bodi ya  Wakurugenzi wa Shirika la  Madini la Taifa (STAMICO)  kwa kushirikiana  na menejimenti  ya Mgodi wa STAMIGOLD kuwasilisha mpango wa kibiashara wenye kuainisha gharama za uzalishaji, mapato na faida.

“ Tunataka kuanzia sasa STAMIGOLD uwe ni mgodi wa mfano wenye kuzalisha kwa faida Tanzania, badala ya kufanya kazi kwa mazoea,” alisema Kairuki.
Katika hatua nyingine, Waziri Kairuki aliutaka Mgodi wa STAMIGOLD  kutumia Wakala wa Jiolojia  Tanzania (GST) kwenye tafiti zake za madini kwa kuwa  wakala huo una  wataalam na maabara za kutosha.

Alieleza kuwa kutokana na wakala huo kuwa na uzoefu katika utafiti wa madini ni muhimu kwa Mgodi wa STAMIGOLD kushirikiana nao kwenye utafiti wa madini kama njia mojawapo ya kuboresha  tafiti zake.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo aliitaka STAMIGOLD  kuwa wabunifu kwa kufanya utafiti na kubaini maeneo  yenye mashapo ya madini ya dhahabu ili kuwa na  miradi endelevu ya uchimbaji madini

Alisema kuwa Serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa sekta ya madini inakuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi, hivyo inaanza na usimamizi wa karibu kwa migodi yote inayosimamiwa na serikali, binafsi na wachimbaji wadogo na kufanyia kazi changamoto mbalimbali zinazojitokeza.

alipongeza ujio wa Waziri na Naibu Waziri wa Madini katika mgodi huo na kuahidi kutekeleza kwa wakati maelekezo  yaliyokuwa yametolewa.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Balozi Alexander Muganda
Alisema pamoja na mgodi kuwa na changamoto nyingi za kiuendeshaji kama bodi watahakikisha wanasimamia masuala ya kiutendaji kwa karibu zaidi, kushauri na kuwasilisha  ripoti za mara kwa mara kwa Waziri na Naibu Waziri wa Madini.

 Wakati huo huo Waziri Kairuki pamoja na Naibu wake Nyongo, walikutana na wafanyakazi  wa Mgodi wa STAMIGOLD Biharamulo ili kusikiliza kero mbalimbali na kuzitatua.
Katika kikao hicho Waziri Kairuki ameelekeza Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la STAMICO pamoja na  uongozi wa Mgodi wa STAMIGOLD Biharamulo kuzingatia maslahi ya watumishi  ikiwa ni pamoja na kupata mishahara kwa wakati, kuwa na bima za afya, kufuata utaratibu wa manunuzi na  kuwepo kwa uwazi kwenye uzalishaji.

Katika kikao hicho ameagiza  bodi hiyo,  kumsimamisha kazi aliyekuwa afisa manunuzi, January Kinunda kwa kushindwa kusimamia mkataba wa ukodishaji wa mashine kwa ajili uchorongaji.
Awali ilielezwa katika kikao hicho kuwa mashine hizo mbili zililetwa kwa dharura huku zikiwa si mpya  ambapo zimekuwa zikiharibika mara kwa mara na kufikia hatua  ya moja kufanya kazi mara moja kwa wiki na kukwamisha uzalishaji katika

No comments:

Post a Comment