Na Rhoda James, Lindi
Naibu
Waziri wa Madini, Doto Biteko amewataka Wachimbaji wa Madini ya
Jasi kuungana ili kuweza kuandaa Kanuni ndogo ndogo kwa ajili
ya kukabiliana na changamoto katika utekelezaji wa shughuli zao
ikiwemo ya Bei ya Madini ya Jasi.
Aliyasema
hayo tarehe 17 Januari, 2018, wakati alipowatembelea Wachimbaji Wadogo
katika ziara ambayo inalenga kutatua migogoro iliyopo katika sekta husika
katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
Naibu
Waziri alisema kuwa bei ya madini ya Jasi imekuwa ikitofautiana kutokana
na kukosekana kwa umoja baina ya wachimbaji wa madini hayo.
“
Jiungeni pamoja mpange bei ya kuuza Jasi kwa pamoja na mkiwa kitu kimoja
changamoto hizi hazitakuwepo,” amesisitiza Biteko.
Pia, Naibu
Waziri alisema kuwa, ameelezwa kuwa ipo changamoto ya miundombinu ya
barabara na hivyo kuitaka Halmashauri ya Kilwa kuangalia namna ya kutatua
tatizo hilo kwa kuwa itatumka kwa shughuli mbalimbali.
Kwa
upande wake Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mayigi
Makolobela alisema kuwa Jasi inayochimbwa katika mikoa ya Lindi na Mtwara ina
ubora wa asilimia 89-95 na iko juu ukilinganisha na Jasi inayopatikana nchi
jirani.
Vilevile, Makolobela
ameeleza kuwa kiwango cha Jasi kilichochimbwa katika kipindi cha Mwezi
Julai hadi Desemba, 2017 kilikuwa Tani 44,500 na gharama yake ilikuwa Shilingi
bilioni 4.6.
Aliongeza
kuwa, katika kiasi hicho cha Jasi kilichopatikana Serikali imekusanya
Mrabaha wa shilingi milioni 138 kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba
2017.
Naye
Mwenyekiti wa Wachimbaji Wadogo wa Jasi Mkoa wa Lindi, Peter Ludvick alimweleza
Naibu Waziri kuwa ikiwa Serikali itawasaidia suala la miundombinu
hususan barabara wachimbaji watazalisha mara tatu ya kiwango
wanachokizalisha hivi sasa.
No comments:
Post a Comment