Wednesday, November 22, 2017

Waziri Kairuki, Nyongo Wakutana Na Femata Geita


Waziri wa Madini, Angellah Kairuki na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (mbele katikati) wakiongoza kikao na baadhi ya  wawakilishi kutoka Shirikisho la  Vyama vya  Wachimbaji Wadogo wa Madini (FEMATA) mkoani Geita 

 Rais wa Shirikisho la  Vyama vya  Wachimbaji Wadogo wa Madini (FEMATA) Taifa,  John Bina (kulia) akieleza jambo katika kikao hicho. Kushoto ni Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo 

 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akifafanua jambo katika kikao hicho 

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo wamekutana na wawakilishi kutoka Shirikisho la  Vyama vya  Wachimbaji Wadogo wa Madini (FEMATA) mkoani Geita lengo likiwa ni kubaini changamoto zao pamoja na kuzitatua. Kati ya maombi yaliyowasilishwa na wawakilishi hao ni pamoja na uwepo wa siku ya maadhimisho ya madini nchini, elimu kuhusu kanuni na sheria mpya za madini, maeneo zaidi kwa ajili ya uchimbaji madini na fidia kwa wananchi waishio ndani ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM)

No comments:

Post a Comment