Na Issa Mtuwa, Gairo
Wachimbaji wa Madini
ya Rubi wilaya ya Gairo kata ya Iyombe kijiji cha Kirama, wamekimbia na kutelekeza
Madini ya viwandani aina ya Rubi Nut, Pikipiki na vifaa mbalimbali vya kuchimbia
baada ya kuona msafara wa Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula na Mwenyekiti
wa ulinzi na usalama ambae pia ni Mkuu wa Wilaya (DC) ya Gairo Seriel Shaid
Mchembe waliokuwa wanatembelea mgodi huo kuona shuguli za uchimbaji kwa lengo
la kwenda kutatua kero zinazowakabili.
Msafara wa mwenyekiti
wa Tume ya madini akiwa ameambatana na Kamishna wa Tume hiyo Dkt. Athanas
Machiyeke na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ulianza majira ya saa tatu
asubuhi kuelekea kwenye eneo la mgodi.
Wakiwa njiani msafara
huo ulikubwa na changamoto baada ya gari ya Polisi iliyokuwa inaongoza msafara
huo kukwama kwenye maji katikati ya mto kwa muda wa saa moja kitendo
kilichopelekea kuchelewa kufika kwenye eneo la mgodi.
Hata hivyo mara baada
ya kufika kwenye nyumba ya mchimbaji mmoja alie tambuliwa kwa jina la Sadick
Athuman maarufa kwa jina la (Saadam) alikutwa kijana mmoja aliejitambulisha kwa
jina la Athumani mkazi wa Gairo mjini akilinda mahali apo ndipo mkuu wa Wilaya
na vyombo vyake vya ulinzi na Mwenyekiti wa Tume na Kamishna waliingia ndani na
kufanya msako na kukuta madini aina ya Rubi Nut yakiwa kwenye mifuko, Pikipiki
moja na vifaa mbalimbali vya kuchimbia.
Alipo ulizwa bwana Athumani,
nani anae miliki madini hayo, alisema ni madini ya bwana Saadam. Alipo ulizwa
yeye anafanya nini alisema yeye ni kibarua tuu na mwenyewe Saadam yupo mgodini
anaendelea na uchimbaji ndipo Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama
akamuamuru Athumani kwenda nae mpaka anakochimba bwana Saadam na mara baada ya
kufika eneo la mgodi wachimbaji wote wakakimbia na kuelekea vichakani akiwemo
bwa Saadam huku vifaa vya uchimbaji vikiwa vimetelekezwa sambamba na madini
yale ya kwenye mfuko na pikipiki.
Kufuatia kitendo
hicho mwenyekiti wa tume ya Madini Prof. Kikula amesikitishwa na kitendo hicho
ambacho kinaashiria uchimbaji wa mgodi huo unafanyika bila kufuata sheria.
Kutokana na hali
hiyoo, mwenyekiti wa tume amemuagiza afisa Madini Mkazi mkoa wa Morogoro
Mhandisi Emmanuel Shija kufuatilia uhalali wa eneo hilo (Leseni na Codinates)
na mwenendo mzima wa uchimbaji wake, endapo eneo hilo litakuwa na leseni mmiliki
wake alipe maduhuli yote anayotakiwa kulipa tangu alipoanza na kama eneo hilo
halijakatiwa leseni mgodi huo ufungwe mara moja na shuguli za uchimbaji
zisitishwe mara moja.
Aidha, amesikitishwa
na wachimbaji na wawekezaji katika eneo hilo kushindwa kusaidia shuguli za
maendelo ya kijiji kinacho zunguka migodi hiyo ambapo ofisi yake haikumridhisha
mwenyekiti wa tume.
Kwa upande wake Mkuu
wa wilaya ya Gairo amesikitishwa na wachimbaji hao kwa kukiuka sheria zinazo
ongoza shuguli za uchimbaji madini, amesema amekuwa akiwahimizi mara kadhaa
wachimbaji wote wilayani humo kuzingatia na kufuata taratibu kabla hawajanza
kazi za uchimbaji ikiwemo kukata leseni na kulipa maduhuli ya serikali.
Kufuatia kwa tukio
hilo Mchembe amepiga marufuku kwa mtu yeyote katika wilaya ya Gairo kufanya
shuguli za madini bila kuwa na kibali kutoka tume ya madini.
Wakati huo huo
Mchembe amemuagiza Kamanda wa Polisi wilaya ya Gairo Lugano Piter Mwakisunga kuhakikisha
anamkamata Sadick Athumani ndani ya siku saba na kumfikisha kwenye vyombo vya
sheria.
Wakiwa kwenye mgodi
wa eneo la mwekezaji wa kampuni ya Mofar Holdings (T) Ltd Kamishna wa Tume ya
Madini Dkt. Machiyeke amemsisitiza mwekezaji huyo kuzingatia taratibu na sheria
katika hatua ya kuajiri wafanyakazi na vibarua na manunuzi ya bidhaa kama
muongozo unavyo sema.
Dkt. Machiyeke amesema,
sheria inasisitiza kutoa kipaumbele kwa wananchi waozunguka mgodi na taifa kwa
nafasi kubwa kabla ya kufikiria nje ya eneo hilo na nje ya nchi.
No comments:
Post a Comment