Monday, March 11, 2019

Nyongo abainisha changamoto zinazoikabili sekta ya madini


Na Nuru Mwasampeta,

Licha ya kwamba Wizara ya Madini kuwa miongoni mwa wizara nyeti katika kufikia uchumi wa viwanda, inakutana na changamoto nyingi.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki katika mkutano wa hadhara na wananchi wa jimbo hilo Tarehe 9 Machi, 2019.

Naibu Waziri Nyongo alizitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni pamoja na utoroshwaji wa Madini unaosababisha Taifa kutokupata kodi stahiki, uwepo wa mikataba isiyolinufaisha Taifa, hali mbaya ya wachimbaji wadogo na hali ya wachimbaji kufanya shughuli zao bila kuzingatia suala zima la usalama. 

Pamoja na changamoto hizo, Naibu Waziri Nyongo alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ilifanyia marekebisho ya Sheria ya Madini ya mwaka 2010 mnamo mwaka 2017.

"Mimi pamoja na uongozi wote wa wizara ya Madini tumepewa dhamana kusimamia sheria hiyo ili Madini yaliyopo nchini yanufaishe Taifa na watu wake", alisema Nyongo.

Awali kabla ya mkutano huo, Naibu Waziri Nyongo alifanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika jimbo hilo.


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika eneo ambako ujenzi wa barabara unaendeshwa ili kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama Tawala cha CCM

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akiwasili katika eneo panakojengwa shule na kupokelewa na Diwani wa kata ya Nyalikungu JosephBundara.

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akiwasili katika hospitali ya wilaya ya Maswa na kupokelewa na uongozi wa hospitali ili kujiridhisha na eneo lililochaguliwa kwa ajili ya kujenga wodi ya wanawake 

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akifuatilia hotuba ya Katibu wa CCM wa Wilaya ya Maswa alipokuwa katika mkutano wa hadhara ili kusikilia na kutatua changamoto ya wananchi wa wilaya hiyo

No comments:

Post a Comment