Monday, November 20, 2017

Katibu Mkuu Mpya Madini Ahimiza Uwajibikaji



Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila, amewataka watumishi wa Wizara kuwajibika katika nafasi zao ili wananchi wanufaike na matunda ya kazi zao kama inavyopaswa.
Profesa Msanjila aliyasema hayo jana, Oktoba 30, 2017 baada ya kuwasili rasmi Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma na kupata fursa ya kuzungumza na wafanyakazi.
Alifafanua kuwa, uwajibikaji hupimwa kwa matokeo. “Tutakuuliza umefanya nini katika nafasi yako ili tuweze kupima utendaji wako.”

Aidha, Profesa Msanjila alisisitiza ushirikiano baina ya viongozi na wafanyakazi wote ili kupata matokeo chanya, hivyo kuleta manufaa katika sekta ya madini.
Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa Wizara ya Madini, Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka, aliahidi ushirikiano kutoka kwa wafanyakazi na uwajibikaji katika nafasi zao kama alivyoasa Katibu Mkuu.

Katibu Mkuu Msanjila, alipokelewa na watumishi wakiongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Lusias Mwenda.




No comments:

Post a Comment