Na Issa Mtuwa, Dodoma
Waziri wa madini Doto
Biteko amewataka wafanyakazi wa wizara ya madini pamoja na taasisi zake kufanya
kazi na kutekeleza majukumu yao kwa wakati ili kufikia malengo ya wizara hiyo.
Ameyasema hayo jijini
Dodoma wakati wa kikao chake na viongozi waandamizi wa wizara ya madini na tume
ya madini. Katika kikao hicho pamoja na mambo mengine amezungumzia juu
utekelezaji wa maagizo anayoyatoa na usimamizi wa utekeleza wa maagizo yake.
Ameongeza kuwa anawategemea sana viongozi hao na wafanyakazi wote katika
kufanikisha kazi na malengo ya wizara hiyo.
Ametolea mfano wa
maagizo aliyowahi kuyatoa ni pamoja na ufutwaji wa leseni zisizo hai ndani ya
siku 7 na zingine siku 30 na lile linalo husu mgodi wa North Mara kuhusu
utiririshaji wa maji yenye sumu kwenda kwenye makazi ya wananchi ambapo alitoa
pia siku 30 kuhakikisha maji hayo yanadhibitiwa.
Amewaambia viongozi hao kuwa akishatoa maagizo,
kazi ya kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo ni kazi yao. Amemshukuru na
kumpongeza Mwenyekiti wa Tume Prof. Idris Kikula na tume yake kwa kazi nzuri
wanayoifanya na ziara zake mikoani zimekuwa na tija.
Biteko amesisitiza
kuwa anatambua mchango wa watumishi wote wa wizara yake hivyo amewaomba kuongeza
bidii na kuongeza umakini katika
utekelezaji wa majukumu yao huku wakizingatia weledi na uadilifu.
Kikao hicho
kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, Katibu Mkuu Wizara ya
Madini Prof. Simon Msanjila na Makamishna. Kwa upande wa tume ya madini
waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa Tume Prof. Kikula, Mtendaji mkuu wa
tume ya madini Prof. Shukrani Manya, Mkurugenzi wa Leseni Mhandisi Yahya
Samamba, Mkurugenzi wa Biashara Dkt. Venance Bahati.
Waziri
wa Madini Doto Biteko katikati akiongoza kikao cha kazi na viongo waandamizi wa
wizara ya Madini na Tume ya Madini. Kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Madini
Stanslaus Nyongo na kulia kwake Katibu Mkuu wizara ya Madini Prof. Msanjila
Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akifafanua jambo wakati wa kikao kilichoitishwa na Waziri wa Madini Doto Biteko kilicho fanyika Ihumwa Jijini Dodoma. |
No comments:
Post a Comment