Wednesday, January 9, 2019

Biteko aapishwa kuwa Waziri wa Madini


Na Asteria Muhozya,

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko ameapishwa leo Januari 9 kuwa Waziri wa Madini katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Waziri Biteko aliteuliwa Januari 8 kushika wadhifa huo baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri na kufanya uteuzi wa viongozi mbalimbali wa wizara na taasisi.

Waziri Biteko anachukua nafasi ya aliyekuwa Waziri wa Madini Angellah Kairuki ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji.


Aliyekuwa Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko akiapa mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kuwa Waziri wa Madini, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam. 

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko akikabidhiwa vitendea kazi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli. 

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko akikabidhiwa vitendea kazi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

No comments:

Post a Comment